HABARI MBAYA KWA MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED, MAMA MZAZI WA SERGIO RAMOS



HABARI MBAYA KWA MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED, MAMA MZAZI WA SERGIO RAMOS
CIwEiUAXAAAgOwQ
Mama mzazi wa Sergio Ramos, Paqui Garcia amefanya mahojiano huku akiwa anaendesha gari na kuziambia Camera za TV kwamba; 
Sergio quiere quedarse en el Madrid (Sergio wants to stay in Madrid) yaani Sergio anataka kuendelea kukaa Madrid
 "Sergio quiere quedarse en el Madrid". Habla la MADRE de Sergio Ramos: http://bit.ly/1j5mmes  pic.twitter.com/GOz3qBWgDj
Maneno ya Paqui Garcia yanaweza kuwa kweli, lakini Ramos bado anaweza kujiunga na Man United majira haya ya kiangazi.
Awali Gazeti la Marca lilienda ndani zaidi na kuchunguza mkataba wa Sergio Ramos katika klabu ya Real Madrid ambapo lilifichua kwamba mlinzi huyo anahitaji mshahara wa euro milioni 10 kwa msimu, wakati Real wanataka kumlipa euro milioni 7.5.
Kama ripoti hizo ni kweli, Ramos anaweza kuendelea kusalia Madrid endapo wataongeza dau, lakini kama watashinda, halafu Man United wakafikisha mzigo, basi atatimkia Old Trafford.


Comments