BEKI MATTEO DARMIAN AKUBABALI KUJIUNGA NA MANCHESTER UNITED ...ada ya pauni milioni 12 na mkataba wa miaka minne
Beki Matteo            Darmian amethibitisha kuwa anajiunga na Manchester United            baada ya kukubali dili la mkataba wa miaka minne.
        United imekubali            kuilipa Torino pauni milioni 12.7 lakini zitafika hadi 14.4            kutegemea na namna atakavyong'ara Old Trafford.
        AC Milan, klabu ya            zamani ya Darmian nayo itapokea pauni 287,000 kama asilimia tano ya mauzo hayo            hiyo ikiwa ni kwa mujibu wa mkataba waliouweka wakati            wanamuuza mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25.
        Darmian            ameichezea Italia mechi 13 na kimo chake kinachokaribia futi 6            kitamsaidia Van Gaal kutatua moja ya matatizo yaliyomkabili            msimu uliopita.
        Van Gaal alitaja            sula la vimo vya wachezaji kama moja ya vitu vinavyohitaji            kufanyiwa uwiano kwenye kikosi chake.
        Usajili rasmi wa            Darmian unatarajiwa kutangazwa masaa 24 yajayo.
        Matteo Darmian                akiichezea Italia katika mechi za kufuzu Euro 2016 dhidi                ya Bulgaria mwezi Machi
        Darmian (kulia)                akifunga dhidi Juventus mwezi April
        
Comments
Post a Comment