ARDA TURAN SASA NI RASMI MALI YA BARCELONA LAKINI YUPO HATARANI KUTEMWA NA KABLA YA KUICHEZEA HATA MECHI MOJA





ARDA TURAN SASA NI RASMI MALI YA BARCELONA LAKINI YUPO HATARANI KUTEMWA NA KABLA YA KUICHEZEA HATA MECHI MOJA
Barcelona imefikia makubaliano na Atletico Madrid  ya kumsajili kiungo  Arda Turan kwa pauni milioni 29.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 alikuwa anawaniwa na Chelsea pamoja na Manchester United, laki Barcelona imekuwa mshindi na kumsainisha Turan mkataba wa miaka mitano.

Hata hivyo mchezaji huyo hataweza kuichezea Barcelona hadi Januari mwakani, kutokana na klabu hiyo kupigwa kitanzi cha kusajili na FIFA kutokana na kashfa ya kusajili vijana wadogo.

Katika makubaliano ya Barcelona na Atletico Madrid kuna kifungu kinachoruhusu mchezaji huyo kutemwa na kurudishwa Atletico kabla ya Julai 20 iwapo rais mpya wa Barcelona hatakubali kuidhinisha usajili.

Uchaguzi wa kumpata rais mpya wa Barcelona utafanyika Julai 18 na iwapo mshindi hatakubali usajili wa Turan, basi mchezaji huyo atarejeshwa Atletico Madrid.

Na kama hilo litatokea, Barcelona watapoteza asilimia 10 ya ada waliyoilipa Atletico.
Barcelona posted this                  mocked-up picture of Arda Turan in a club shirt after                  announcing a deal to sign him
Barcelona imetupia picha na namna Arda Turan atakavyoonekana kwenye jezi yao
Arda Turan, pictured in                  action against Athletic Bilbao last season, will join                  Barcelona for £29million
Arda Turan akiwa uwanjani dhidi ya Athletic Bilbao msimu uliopita




Comments