Jerry Muro (kulia) na            Geofrey Mwashiuya wakiwa mbele ya waandishi wa habari leo
        Na Bertha Lumala
        UONGOZI wa Yanga            umesisitiza kuwa ulimsajili kiungo Geofrey Mwashibhuya akiwa            mchezaji huru.
        Akizungumza na waandishi            wa habari kwenye ofisi za makao makuu ya klabu hiyo jijini Dar            es Salaam leo asubuhi, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano            ya Yanga, Jerry Muro, amesema kuwa Mwashiuya hakuwa na mkataba            na klabu yoyote kabla ya kutua Jangwani.
        "Kuna maneno mengi            yanasemwa juu yetu na usajili wa mchezaji Mwashibhuya. Ukweli            ni kwamba kabla ya sisi (Yanga) kumsajili, hakuwa na mkataba            na klabu yoyote," amesema Muro na kueleza zaidi:
        "Pia taratibu za usajili            zinasema kuwa mchezaji wa timu ya Ligi Daraja la Kwanza nchini            mkataba wake unafika kikomo mara tu ya msimu husika            kumalizika.
        "Mwashiuya alikuwa hapa            kwetu tangu Oktoba mwaka jana, lakini amesaini mkataba wa            miaka mitatu hivi karibuni."
        Kiungo huyo aliyekuwa            amefuatana na Muro katika mkutano na waandishi wa habari, pia            amesisitiza hakuwa na mkataba wowote na klabu nyingine klabu            ya kutia saini kwa mabingwa haoa mara 25 wa Tanzania Bara.
        Kauli ya Yanga imetolewa            ikiwa ni siku chache baada ya uongozi wa Kimondo FC, ambayo            Mwashibhuya aliitumikia, kudai kuwa klabu hiyo ya Jangwani            haikufuata taratibu stahiki za usajili katika kumnasa mchezaji            huyo.
        Mwashiuya aliyezaliwa            Desemba 27, 1996 jijini Mbeya, alionyesha kiwango kizuri            katika mechi ya kimataifa ya kirafiki ya Yanga dhidi ya SC            Villa ya Uganda iliyomalizika kwa suluhu kwenye Uwanja wa            Taifa jijini Jumamosi.
        SHEREHE ZAZINDULIWA
        Katika hatua nyingine,            Muro amesema kuwa uongozi wa Yanga umezindua rasmi sherehe za            kuadhimisha miaka 80 tangu kuanzishwa kwa klabu hiyo ambazo            kilele chake kitakuwa Jumamosi kwenye viwanja vya Jangwani            jijini.
        Amesema Jumamosi kutakuwa            na hafla kubwa itakayochagizwa na shrehe za ubingwa wa 25 wa            Tanzania Bara.
        Yanga ilianzishwa 1935 na            kwa sasa ndiyo timu kongwe zaidi nchini inayoshiriki Ligi Kuu            Tanzania Bara.
        
Comments
Post a Comment