ROY KEANE ASEMA KAMA MITANDAO YA KIJAMII INGEKUWEPO ENZI ZAO BASI ANGEISHIA JELA ...adai mazoezi ya Man United yalikuwa na ushindani kuliko mechi za Premier League


ROY KEANE ASEMA KAMA MITANDAO YA KIJAMII INGEKUWEPO ENZI ZAO BASI ANGEISHIA JELA ...adai mazoezi ya Man United yalikuwa na ushindani kuliko mechi za Premier League
Nahodha wa zamani wa Manchester United, Roy Keane ameponda maisha ya sasa ya wanasoka ambao wengi wanakesha kwenye mitandano ya kijamii.
Roy Keane anasema kama  kama mitandao hiyo ingekuwepo enzi zake za uchezaji soka basi angeishia jela.
"Kama kungekuwa na mitandao ya kijamii enzi zangu, basi ningeishia jela," anasema Roy Keane bila kufafanua.
Kiungo huyo aliyekuwa mtukutu uwanjani anasema enzi hizo mazoezi ya Manchester United yalikuwa yana ushindani kuliko mechi zenyewe.
Wakati wa enzi za Roy Keane miaka ya 90 na mwanzoni mwa 2000, wapinzani wakubwa wa Manchester United kwenye ligi walikuwa ni Blackburn, Arsenal na baadae Chelsea lakini Keane anasema ubora wa kikosi cha United kilipelekea mazoezi yawe na ushindani mkubwa kuliko mechi.
"Jumamosi (siku za mechi) ilikuwa ni kama mapumziko kwetu kwani mazoezi ndio kilikuwa kitu kigumu zaidi," anaeleza Keane aliyeshinda mataji saba ya Premier League na manne ya FA Cup ndani ya Old Trafford.
Keane anasema wanasoka  vijana wa siku hizi kila siku utawaona kwenye mitandao ya kijamii wakitupia picha zao za kujirusha, kitu ambacho amedai hakina manufaa yoyote kwenye soka.
Roy Keane won seven                    Premier League titles in his time at Manchester                    Untied 
Roy Keane alishinda mataji saba ya Premier League katika muda wake ndani ya Manchester Untied 
Keane says training at                    Manchester United was more competitive than matches 
Keane anaemia mazoezi ya  Manchester United yalikuwa na ushindani kuliko mechi zenyewe
Keane arrives at the                    charity event in Dublin where he speaks to a fan in an                    Ireland shirt
Keane akizungumza na shabiki aliyevalia jezi ya  Ireland 
Keane and                    Arsenal's Patrick Viera enjoyed some battles over the                    years, but the United man says training was more                    competitive than matches
Keane na Patrick Viera wa Arsenal walikuwa wapinzani wa jadi lakini Roy Keane bado anasema mazoezi ya United yalijaa ushindani kuliko mechi za ligi





Comments