Roberto Firmino amepiga picha na jezi ya Liverpool kwa mara ya kwanza tangu aliposajiliwa na timu hiyo na kuwa mchezaji ghali wa pili katika historia ya klabu hiyo.
Kiungo mshambuliaji huyo amekamilisha usajili wake wa kwenda Liverpool kwa ada ya pauni milioni 29 kutoka Hoffenheim ya Ujerumani na ametambulishwa rasmi huko Chile mbele ya mtendaji mkuu wa Liverpool Ian Ayre.
Mkali huyo wa kimataifa wa Brazil mwenye umri wa miaka 23, amekubali mkataba wa miaka mitano na mshahara wa pauni 100,000 kwa wiki.
Roberto Firmino yuko na timu ya taifa ya Brazil huko Chile katika michuano ya Copa America.
Roberto Firmino completed amekamilisha usajili wake Liverpool na akapozi na jezi ya timu hiyo kwa mara ya kwanza
Firmino anakuwa mchezaji ghali wa pili katika historia ya Liverpool
Comments
Post a Comment