PETER SCHMEICHEL ATOA LA ROHONI KUHUSU DAVID DE GEA




PETER SCHMEICHEL ATOA LA ROHONI KUHUSU DAVID DE GEA Mlinda mlango wa zamani wa Machester United PETER SCHMEICHEL amesema ataumia sana kuona David De Gea anaondoka Old Trafford kwaajili ya Real Madrid kwa sababu anaamini kipa huyo wa Hispania angestahili kufikia mafanikio yake Manchester United.
Schmeichel alinyanyua mataji makubwa 11 katika kipindi chake alichoichezea United huku De Gea akiwa amenyakua taji moja tu la Premier League msimu wa 2012/13.
Man Utd              legend reveals why he would be UPSET if David De Gea leaves              for Real Madrid
MAUMIVU: Peter Schmeichel hataki kuona David De Gea akiondoka Manchester United
"Sioni sababu ya yeye kushindwa kufikia mafanikio yangu kama atakaa United kwa maisha yake yote ya soka"
Peter Schmeichel
Schmeichel, 51, anafikiri De Gea bado ana nafasi ya kubeba mataji mengi na Machester United kama itakavyokuwa kwa Real Madrid.
Gwiji huyo wa United ameliambia gazeti la The Sun: Nitasikitika kama ataondoka kiangazi hiki kwa sababu ana nafasi ya kuichezea Manchester United mechi nyingi na kushinda mataji mengi kuliko mimi.
"Ni mlinda mlango madhubuti na umri bado wake bado unamruhusu sana, sioni sababu ya yeye kushindwa kufikia mafanikio yangu kama atakaa United kwa maisha yake yote ya soka"
De Gea ameonyesha wazi kuwa anataka kwenda Real Madrid na amekataa kusaini mkataba mpya Old Trafford.


Comments