Klabu ya Guangzhou Evergrande imemsajili kiungo wa Tottenham Paulinho kwa pauni milioni 9.8 huku Mbarazil huyo akianguka mkataba wa miaka minne.
Paulinho anakuwa mchezaji wa kwanza mwenye jina kubwa kuondoka Tottenham katika kipindi hiki ambacho kocha Mauricio Pochettino anataka kukifumua kikosi chake.
Kiungo huyo sasa anakwenda kuungana na kocha wa zamani wa Brazil Luiz Felipe Scolari ambaye ndie kocha mkuu wa klabu hiyo Guangzhou Evergrande.
Paulinho, 26 ameshindwa kudumisha kiwango chake alichokuwa nacho wakati anajiunga na Tottenham kwa pauni milioni 17 miaka miwili iliyopita.
Guangzhou Evergrande ya china imemsajili Paulinho kwa pauni milioni 9.8
Paulinho (kulia) enzi zake akiwa na Tottenham
Luiz Felipe Scolari kocha wa Guangzhou Evergrande
Comments
Post a Comment