PAULINHO WA TOTTENHAM ATIMKIA GUANGZHOU EVERGRANDE YA CHINA




PAULINHO WA TOTTENHAM ATIMKIA GUANGZHOU EVERGRANDE YA CHINA
Klabu ya Guangzhou Evergrande imemsajili kiungo wa Tottenham Paulinho kwa pauni milioni 9.8 huku Mbarazil huyo akianguka mkataba wa miaka minne.

Paulinho anakuwa mchezaji wa kwanza mwenye jina kubwa kuondoka Tottenham katika kipindi hiki ambacho kocha Mauricio Pochettino anataka kukifumua kikosi chake.

Kiungo huyo sasa anakwenda kuungana na kocha wa zamani wa Brazil Luiz Felipe Scolari ambaye ndie kocha mkuu wa klabu hiyo Guangzhou Evergrande.

Paulinho, 26 ameshindwa kudumisha kiwango chake alichokuwa nacho wakati anajiunga na Tottenham kwa pauni milioni 17 miaka miwili iliyopita.
Chinese club Guangzhou                    Evergrande have signed Tottenham midfielder Paulinho                    for a £9.8million fee
Guangzhou Evergrande ya china imemsajili Paulinho kwa pauni  milioni 9.8 
Paulinho (right) struggled                    to make an impact at Tottenham during his two seasons                    at the club
Paulinho (kulia) enzi zake akiwa na Tottenham
The 26-year-old will                    reunite with ex-Brazil boss Luiz Felipe Scolari -                    after he was appointed earlier this month
 Luiz Felipe Scolari kocha wa Guangzhou Evergrande 




Comments