PATRICK VIEIRA amemfagilia Raheem Sterling na kuwaponda wanaosema ni ujinga kwa Manchester City kumnunua winga huyo kwa zaidi ya pauni milioni 40.
Mabosi wa Etihad Stadium wanatajwa kutenga pauni milioni 50 kwa nyota huyo wa Liverpool baada ya ofa zao za pauni milioni 30 na 40 kupigwa chini.
Hiyo itamfanya Sterling awe mchezaji ghali zaidi Uingereza kuliko yeyote yule huku baadhi ya watu wakisema hana thamani hiyo.
Lakini Viera ambaye kwa sasa ni anangoza academy ya City, amesema winga huyo wa kimataifa wa England ana vigezo vyote vya kununuliwa kwa bei mbaya.
Comments
Post a Comment