Mabosi wa              Manchester United wameisisitizia Real Madrid kuwa  De Gea              hatauzwa labda tu kama watapewa Sergio Ramos.
          Rais wa Real Madrid,                  Florentino Perez sasa anasema Ramos thamani yake ni                   pauni million 40 na anataka wapewe De Gea pamoja na                  pauni milioni 20 kutoka United. 
          Mwanzoni ilisemwa Real                  wanamtaka De Gea na pauni milioni 40 huku Perez                  akimthaminisha Ramos kwa pauni milioni 145.
          Lakini mtendaji mkuu wa                  Manchester United Ed              Woodward anajua ni jinsi gani Perez amepania kumpata De Gea              kiangazi hiki na hivyo amepanga kuwakomalia miamba hiyo ya              Hispania.
          Daily Star la              Uingereza linaandika kuwa United ipo tayari kumuona De Gea              anamalizia mkataba wake wa miezi 12 iliyobakia iwapo Real              Madrid watakataa kufuata matakwa yao.
          Licha ya kuwa De              Gea, 24 atakuwa huru kiangazi kijacho lakini United inaamini              Real Madrid watakuwa na kipa huyo kwa miaka 10 ijayo huku              thamani yake ikizidi kuongezeka. 
          Kimahesabu,              United inaona kumnunua Ramos kwa bei mbaya ni hasara              kwasababu beki huyo mwenye umri wa miaka 29 atakuwa hana              thamani pindi mkataba wake utakapomalizika Old Trafford.
          United ina jeuri ya pesa na hivyo haiofii kuendelea kukaa                na De Gea kwa mwaka mmoja zaidi na kumwacha aondoke bure                na kupoteza pauni milioni 20 ambazo ingezipata kwa                kumuuza. 
        Ramos anabanwa na mkataba lakini              inadaiwa ameshawaambia  Real kuwa anataka kutimka.
          Barcelona ilionyesha nia ya              kumtaka Ramos lakini Perez akakataa kumuuza sentahafu huyo              kwa wapinzani wao wakubwa.
          Hiyo inazidi kuwapa jeuri United              ambayo sasa imewaachia Real Madrid waamue kusuka au kunyoa.
          
Comments
Post a Comment