LIVERPOOL YATHIBISHA KUMSAJILI ROBERTO FIRMINO …yampa mkataba wa miaka mitano, mshahara pauni 100,000 kwa wiki
Liverpool imethibitisha kumsajali kiungo mshambuliaji Roberto Firmino kwa ada ya pauni milioni 29 akitokea Hoffenheim ya Ujerumani.
Klabu hiyo imesema mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil mwenye umri wa miaka 23 amekubali mkataba wa miaka mitano kwa mshahara wa pauni 100,000 kwa wiki.
Kilichobakia sasa ni kukamilishwa kwa hati za kufanyia kazi pamoja na vipimo vya afya kabla ya mchezaji huyo kutangazwa rasmi.
Kiungo mshambuliaji Roberto Firmino amekamilisha usajili wa pauni milioni 29 kwenda Liverpool
Firmino akiwa mazoezini na Brazil huko Santiago Chile
Firmino, 23 (kulia) aanaondoka Hoffenheim ya German na kujiunga na Liverpool
Manchester United ambayo msimu uliopita ilipwaya sana kwenye eneo la kiungo, ilikuwa ikimfuatilia kwa karibu Firmino baada ya kuvutiwa na kiwango chake kwenye Bundesliga msimu uliomalizika.
Wiki kadhaa, nyuma tetesi zilisema Firmino anatarajiwa kwenda Old Trafford kufanya vipimo vya afya mara tu Copa America itakapomalizika, lakini Liverpool wamekuwa wababe zaidi.
Liverpool watalipa pauni milioni 22 mwanzoni na kiasi kilichobakia kitalipwa baadae.
Comments
Post a Comment