LIVERPOOL YAIFANYIA KITU MBAYA MANCHESTER UNITED …yamsajili Roberto Firmino kwa pauni mil 29



LIVERPOOL YAIFANYIA KITU MBAYA MANCHESTER UNITED …yamsajili Roberto Firmino kwa pauni mil 29
LIVERPOOL imeipiga bao la kisigino Manchester United baada ya kufikia maafikino ya kumsaji kiungo 'mtamu' wa Brazil Roberto Firmino kwa ada ya pauni milioni 29.
Dili hilo litakamilika Jumatano ambapo kiungo huyo wa Hoffenheim ya Ujerumani, atakuwa mchezaji wa pili wa bei mbaya kusajiliwa na Liverpool.
Andy Carroll  aliyesajiliwa kwa pauni milioni 35 miaka kadhaa iliyopita kabla ya kupigwa bei baadae, ndiye anayeendelea kushikilia rekodi ya usajili wao wa bei mbaya Liverpool.
Mtendaji mkuu wa  Liverpool Ian Ayre alikuwa Chile Jumanne kwaajili ya kujaribu kukamilisha usajili wa Firmino anayeitumikia Brazil kwenye michuano ya Copa America inayoendelea huko Chile.
Roberto              Firmino
DILI LIMEKAMILIKA: Liverpool imeshinda mbio za kumsajili Roberto Firmino
"Ni wakati wa kutafuta changamoto mpya katika maisha yangu ya soka"
Roberto Firmino
Wawakilishi wa Firmino pia wako Chile kufuatilia nyendo zote za mteja wao.
Firmino hivi karibuni alisema kuwa yupo tayari kutafuta changamoto mpya kwenye maisha yake ya soka ambapo alisema: "Ni wakati muafaka wa kupiga hatua nyingine, lakini kwasasa akili yangu yote ipo kwa Brazil kwenye michuano ya Copa America."
Manchester United ilikuwa ikimfuatilia kwa karibu kiungo huyo ambaye ametokea kuwa bidhaa adimu kutokana na soka yake safi aliyoionyesha kwenye Bundesliga msimu uliomalizika.
Wiki kadhaa, nyuma tetesi zilisema Firmino anatarajiwa kwenda Old Trafford kufanya vipimo vya afya mara tu Copa America itakapomalizika, hali iliyoashiria kuwa safari ya kwenda Manchester United kwa kiungo huyo bingwa wa kukokota mpira, ilikuwa imeiva.


Comments