LIVERPOOL YAELEKEZA NGUVU KWA MARIO GOMES 'MUUAJI' WA FIORENTINA



LIVERPOOL YAELEKEZA NGUVU KWA MARIO GOMES 'MUUAJI' WA FIORENTINA

LIVERPOOL imeingia sokoni kusaka straika mpya na rada zao sasa zimenasa kwa Mario Gomez wa Fiorentina ambaye kwa mujibu wa mtandao wa Tuttomercatoweb anataka kuondoka Serie A baada ya kuona makali yake yanapungua.

Straika huyo wa kimataifa wa Ujerumani, amefanikiwa kufunga mabao 10 tu msimu uliomalizika, lakini anabaki kuwa staa tishio kwenye 18 za adui – sifa aliyokuwa nayo tangu anaibuka hadi sasa.

Gomez mwenye umri wa miaka 29, hadi sasa amepiga mabao ya kuvutia 166 katika ligi ndani ya mechi 308 alizocheza kwa kipindi chake chote.


Comments