Morgan Schneiderlin ameonekana akiwasili Southampton tayari kwa mazoezini ya kujiandaa na msimu mpya licha            ya kiungo huyo Ufaransa kuwa mbioni kutua Manchester United            kwa pauni milioni 25.
        Mkali huyo mwenye umri wa miaka 25 amepigwa            picha Jumatatu akiwasili mazoezini akiwa sambamba na mchezaji            mpya aliyesajiliwa kiangazi hiki Maarten Stekelenburg.
        Kikosi cha Southamton kimeanza mazoezi            mapema Jumatatu hii tayari kwa kujiandaa na michuano ya Europa League mwishoni mwa mwezi Julai.
        Schneiderlin anatarajiwa kutangazwa rasmi            kujiunga na Manchester United wiki hii.
        Morgan Schneiderlin (kushoto)                akiwasili kwenye uwanja wa wazoezi wa  Southampton akiwa                sambamba na mchezaji mpya Maarten Stekelenburg
        Kiungo wa                Southampton Schneiderlin anatarajiwa kujiunga na                Manchester United
        Schneiderlin                alinyimwa kuondoka St Mary msimu uliopita lakini safari                hii klabu yake imekubali kumuuza
        
Comments
Post a Comment