KUNA UWEZEKANO MKUBWA WA VAN PERSIE KUONDOKA MANCHESTER UNITED


KUNA UWEZEKANO MKUBWA WA VAN PERSIE KUONDOKA MANCHESTER UNITED


Mshambuliaji wa Manchester United Robin van Persie anaweza akaondoka Old Trafford kiangazi hiki.
Mchezaji huyo wa zamani wa Arsenal aliyejiunga na Manchester United kiangazi cha mwaka 2012, alishindwa kuwa namba ya kudumu chini ya Loius van Gaal msimu uliopita na akatumia muda mwingi kama chaguo la pili nyuma ya Wayne Rooney.
Mapema wiki hii, Van Persie, 31 amegusia kuwa anaweza akaondoka Old Trafford kama hata hakikishiwa namba ya kudumu.
Kwa mujibu wa mtaalam wa soka wa Holland, Marcel van der Kraan, kuna uwezekano mkubwa mshambuliaji huyo akaondoka Manchester United kiangazi hiki.
"Uwezekano wa yeye kuondoka ni mkubwa, ndio ni mkubwa sana," Van der Kraan ameliambia gazeti la Daily Star.
SAFARI INANUKIA: Van Persie kuondoka United asipohakikishiwa namba ya kudumu
"Uwezekano wa Van Persie kuondoka ni mkubwa"
Marcel Van der Kraan
Van der Kraan anaeleza zaidi: "Niliongea na Van Persie wiki chache zilizopita na akaniambia atakutana na Louis van Gaal na kujadili juu ya hatma yake.
"Nikamuuliza hiyo ina maana gani, akaniambia ni kwamba tu anataka kujua hatma yake ndani ya Manchester United.
"Nadhani hataki suala la kuwa mtu kwa kusota benchi. Anataka kucheza, sio tu kwaajili ya kulinda nafasi yake kwenye Euro 2016 bali anataka kucheza zaidi na zaidi.
"Hadhani kama kukaa benchi kwaajili ya kusubiri eti awe fiti kutasaidia soka lake.
"Hiyo ndio sababu akataka kucheza mechi za 'marizevu' dhidi ya Fulham na Leicester msimu uliopita".
Robin van Persie has                    reiterated his desire for regular football as he                    considers Manchester United future
Robin van Persie ameeleza utashi  wa kupata uhakika wa namba ya kudumu wakati akitathmini hatma yake Manchester United 
Van Persie is currently on                    holiday in Miami with wife Bouchra and his children as                    they enjoy a family holiday
Van Persie kwa sasa yupo likizo  huko Miami akiwa na mkewe Bouchra pamoja na watoto wao
Van Persie and his wife                    Bouchra are all smiles as they catch the sun in Miami                    while on a breakĀ 
Van Persie na mkewe Bouchra wakifurahia mapumziko

TAKWIMU ZA VAN PERSIE NDANI YA MAN UNITED

2012-13: magoli 26 katika mechi 38 
2013-14: magoli 12  katika mechi 21 
2014-15: magoli 10 katika mechi 27 
Van Gaal alishasema hivi karibuni kuwa Manchester haina mpango wa kumuuza Van Persie na kwamba yupo kwenye mipango yake ya msimu ujao.

Hata hivyo kocha huyo alimtaka Van Perisie akaze buti mazoezi na kudhihirisha kuwa yupo fiti, vinginevyo atajikuta akikaa benchi.


Comments