KISIGA AANGUKA MMOJA KWA WANAJESHI….


KISIGA AANGUKA MMOJA KWA WANAJESHI….

Kisiga--November7-2014

Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Simba, Shaaban Kisiga 'Malone' amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia klabu iliyoshuka daraja msimu uliopita, Ruvu Shooting ya Mlandizi, Pwani.

Kisiga ambaye aliachwa na Simba mwanzoni mwa msimu uliopita kwa madai ya utovu wa nidhamu, ameamua kuanza maisha mapya na Wanajeshi hao ambao wanajipanga kuhakikisha wanarudi ligi kuu ndani ya mwaka mmoja.

Kisiga kabla ya kutua Simba alikuwa anakipiga Mtibwa Sugar ambayo kwasasa imegoma kumrejesha.



Comments