Kama kama kweli Barcelona wanahitaji            kumsajili mshambuliaji wa Manchester United, Angel Di Maria            basi italazimika kulipa pauni milioni 85.5.
        Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina hana            furaha Old Trafford baada ya kuanza vibaya kwa msimu wake wa            kwanza Manchester United.
        Imebainika kuwa wakati Real Madrid inamuuza            Di Maria kwa Manchester United, iliweka kipengele kinachomzuia            mchezaji huyo kurejeshwa Hispania kwa ada iliyo chini ya pauni            milioni 85.5.
        Kwahiyo ili Barcelona imnase mkali huyo ni            lazima ivunje benki na kulipa pauni milioni 85.5.
        Bayern Munich pia ilikuwa inamtaka Di Maria            lakini sasa imehamishia nguvu zake kwa Douglas Costa wa Shakhtar Donetsk ambaye            anawaniwa pia na Chelsea.
        Barcelona watalazimika              kulipa £85million kama kweli wanataka kumsajili mshambuliaji              wa Manchester United  Angel di Maria
        Di Maria amekiri hakuwa              na msimu mzuri Manchester United 
          
Comments
Post a Comment