Graphic kutoka kwa            mchambuzi mmoja wa soka imesambaa kwenye mitandao ikionesha            mfumo mpya wa Liverpool wanaoweza kutumia msimu wa 2015-16            ambao ni 3-4-3.
        Kikosi hicho cha            Liverpool kimewashangaza wengi kutokana na Nathaniel Clyne            kuanzishwa upande wa kushoto.
        Clyne, ambaye anatarajia            kukamilisha usajili wa kujiunga na Liverpool kutokea            Southampton kwa dau la paundi milioni 12.5 ni beki wa kulia            kiasilia, lakini kaanza sehemu tofauti.
        Mchambuzi huyo amejaribu            kadri awezavyo kuwaingiza kwenye kikosi cha kwanza wachezaji            wapya wa Liverpool na amependekeza kwamba,  Danny Ings anaweza            kucheza mbele na  Daniel Sturridge, huku Roberto Firmino,            Jordan Henderson na  Philippe Coutinho wakicheza safu ya            kiungo.
        Wakati huo huo,  James            Milner, aliyejiunga na Liverpool kutoka Man City akipangwa            kucheza kwa mapana kutoka winga ya kulia, huku kushoto            akipangwa   Alberto Moreno.
         Adam Lallana hajapata            nafasi ya kuanaza.
        Tazama Graphic hapa chini            ikionesha kikosi cha kwanza cha Liverpool;
        
Comments
Post a Comment