GONZALO HIGUAIN HAUZIKI …ARSENAL, LIVERPOOL, MAN CITY NI LAZIMA WALIPE PAUNI MILIONI 67



GONZALO HIGUAIN HAUZIKI …ARSENAL, LIVERPOOL, MAN CITY NI LAZIMA WALIPE PAUNI MILIONI 67
Napoli imedhamiria kubaki na mshambuliaji wao Gonzalo Higuain huku ikisema hakuna klabu inayoweza kumng'oa bila pauni milioni 67 ambacho ndicho kipengele kilichowekwa kwenye mkataba wake.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentina ambaye kwasasa yupo Chile akiitumikia nchi yake kwenye michuano ya Copa America, amekuwa akiwaniwa na Liverpool, Arsenal, Manchester City pamoja na AC Milan.  
Msemaji wa Napoli Nicolas Lombardo amesema hakuna nafasi ya Higuain kuondoka labda timu zifikie kipengele hicho cha pauni milioni 67.
"Napoli tumedhamiria kuweka wazi hili kwa kutoa mwongozo rasmi kwamba Higuan ana kipengele cha manunuzi cha pauni milioni 67.
"Hakuna ofa itakayopokelewa chini ya kiwango hicho, wote wanaomtaka mchezaji huyo ni lazima wafikie thamani yake," anaeleza Lombardo katika maongezi yake na Radio Kiss Kiss ya Italia.
Napoli are keen to keep                    hold of star striker and Argentina                    international Gonzalo Higuain
Napoli hawana mpango wa kumuuza mchezaji wa kimataifa wa Argentina Gonzalo Higuain mwenye umri wa miaka 27
Higuain has a £67million                    release clause written into his contract and Napoli                    are sticking by that  
Higuain anakipengele kinachomrushu kuondoka Napoli kwa pauni million 67


Comments