EDINSON CAVANI ‘AIPELEKA’ CHILE NUSU FAINALI YA COPA AMERICA …YAICHAPA URUGUAY 1-0, MAURICIO ISLA AIBUKA SHUJAA



EDINSON CAVANI 'AIPELEKA' CHILE NUSU FAINALI YA COPA AMERICA …YAICHAPA URUGUAY 1-0, MAURICIO ISLA AIBUKA SHUJAA
Cavani is shown the red card by            referee Ricci after a second yellow was deemed the correct            punishment for a touch to Jara's face
Mchezo wa kwanza wa robo fainali ya Copa America, ukashuhudia dakika 80 za mwanzo wenyeji Chile wakiibana Uruguay lakini wakakosa kabisa mbinu za kutupia mipira wavuni.

Wakati hatua ya matuta ikianza kunukia kwenye jiji la Santiango, Chile wakafanikiwa kuweka hai ndoto zao za kutwaa taji kubwa baada ya miaka mingi.

Mshambuliaji tegemeo wa Uruguay Edinson Cavani akafanya makosa mawili ya kijinga yaliyosababisha alambwe kadi mbili za njano zilizozaa kadi nyekundu dakika ya 63 na kuwapa ahueni kubwa wenyeji.

TIMU ZILIVYOKUWA

Chile (4-3-1-2): Bravo 7; Isla 7, Medel 6.5, Jara 7, Mena 6.5; Aranguiz 7, Diaz 6.5 (Fernandez 71 mins, 6), Vidal 6.5; Valdivia 8.5 (Pizarro 85); Sanchez 7.5, Vargas 6.5 (Pinilla 71, 6).

Uruguay (4-4-2): Muslera 7; Pereira 6, Gimenez 7, Godin 7, Fucile 5; Sanchez 5.5 (J Rodriguez 85); Rios 6, Gonzalez 6.5, C Rodriguez 6.5, Rolan 5.5 (Hernandez 58, 6), Cavani 4.

Uruguay walicheza zaidi mchezo wa kujihami huku wakiweka ukuta mgumu uliowatesa vijana  Jose Sampoli lakini dakika 81 Mauricio Isla aliyewahi kuichezea QPR ya England kwa mkopo akaifungia Chile bao pekee.

Wakati mpira ukielekea ukingoni, Uruguay wakalambwa kadi nyingine nyekundu baada ya Jorge Fucile kutolewa kwa kumchezea rafu ya hatari  Alexis Sanchez.
Chile wanatinga nusu fainali ambapo sasa watachuana na mshindi wa mchezo wa Bolivia na Peru utakochezwa Ijumaa.

Wenyeji wanapewa nafasi kubwa ya kutinga fainali na kukabialiana kati ya Argentina, Colombia, Brazil au Paraguay.


ROBO FAINALI ZILIZOBAKIA

Friday, June 26, 00:30 - Bolivia vs Peru
Sat, June 27, 00:30 - Argentina vs Colombia
Sat, June 27, 22:30 - Brazil vs Paraguay 


Mauricio Isla (centre)                  celebrates with the Chile substitutes after he found the                  net to score a late winner for the hosts in Santiago
Mauricio Isla (katikati) akishangilia na wachezaji wa akiba wa  Chile baada ya kuifunga bao pekee
Isla slams in the winner to                  settle the tie as Uruguay's despairing defenders try to                  dive in to stop him scoring - in vain
Isla akifunga goli dakika ya 81
Uruguay striker Edinson                  Cavani was shown a red card for two yellows after                  abusing the referee's assistant and a flick at Gonzalo                  Jara
Edinson Cavani akilambwa kadi nyekundu
Cavani makes his                  disagreement very clear as he argues with former West                  Bromwich Albion defender Jara over his reaction to the                  touch
Cavani akionyesha kukerwa na maamuzi



Comments