KOCHA wa Atletico Madrid, Diego Simeone, amesema Manchester United inaweza kukamilisha uhamisho wa mshambuliaji Mario Mandzukic.
Simeone amedai kwamba Atletico Madrid haina mpango wa kumzibia njia mshambuliaji wake huyo asikamilishe uhamisho wake kwenda United.
Kocha huyo raia wa Argentina anaamini kuna wachezaji wawili tu ambao klabu yake haitawapiga bei na kwamba kuondoka ama kubaki kwa Mandzukic si juu yake.
"Klabu itaamua kipi bora. Tunafurahia kuwa na Mandzukic, alikuwa na kampeni ya ushindani sana. Bila shaka hapa Atletico kuna wachezaji wachache ambao hawawezi kuguswa: Koke, Godin na kuhusu hao ningesema," alisema.
United imekuwa ikihusishwa na uhamisho wa pauni milioni 36 wa Mandzukic.
Comments
Post a Comment