Paraguay ikiwa imepewa nafasi finyu ya kufika nusu            fainali ya Copa America, imefanya kisichotarajiwa baada ya            kuitupa nje Brazil. 
        Katika mchezo huo wa robo fainali timu hizo zilitoshana            nguvu kwa sare ya 1-1 pale dakika 90 za kawaida zilipotimu na            hivyo njia ya mikwaju ya penalti ikachukua nafasi yake.
        Paraguay wakatupia wavuni michomo minne huku wakipoteza            moja wakati Brazil walikosa penalti mbili na kupata tatu na            hivyo kutolewa kwa jumla ya penalti 3-4.
        Brazil ilikuwa ya kwanza kutangulia kwa bao la dakika            ya 15 lililofungwa na mshambuliaji wao mzoefu Robinho.
        Dakika ya 72, Paraguay            wakapata penalti iliyopigwa vizuri na Derlis Gonzalez na kuzaa            bao la kuzawazisha.
        Paraguay sasa itakutana na Argentina katika mchezo wa            fainali utakaopigwa Jumanne wakati nusu fainaili nyingi            itaikutanisha Chile na Peru siku ya Jumatatu.
        
Comments
Post a Comment