CHILE YATANGULIA FAINALI, YAISUBIRI ARGENTINA AU PARAGUAY ...tazama picha kibao namna walivyoichinja Peru



CHILE YATANGULIA FAINALI, YAISUBIRI ARGENTINA AU PARAGUAY ...tazama picha kibao namna walivyoichinja Peru
Guerrero attempts to hold the ball up as Gary Medel              (right) and Marcelo Diaz (left) mark him tightly

Nchi mbili pinzani zilizowahi kupigana vita vya Pacific karne ya 19, Chile na Peru zilikuwa na vita nyingine katika nusu fainali ya Copa America ambapo wenyeji wamesonga mbele kwa ushindi wa bao 2-1.

Hata hivyo mchezo huu unaacha mjadala mkubwa baada ya Chile kuonyesha soka bovu kabisa tangu michuano hii ianze lakini kwa kile kilichoonekana kama mbeleko ya refarii, timu hiyo ikatinga hatua ya fainali na sasa inasubiri mshindi kati ya Argentina na Paraguay.

Kitendo cha mwamuzi Jose Argote kumlamba kadi nyekundu Carlos Zambarano nacho kitachochea utambi katika mjadala mkubwa mingoni mwa mashabiki wa soka wa Peru.

Jose Argote alimpa kadi ya njano Zanbarano kunako dakika ya 7, kabla ya kumtoa nje dakika ya 20, hatua iliyochangia Chile kupata bao la kwanza kupitia Eduardo Vargas katika dakika ya 42.

Ingawa huwezi kumlamu Jose Argote kwa kumtoa Zambarano   baada kumkanyaga mgongoni Charles Aranguiz, mwamuzi alikuwa na matukio mengi yaliyozua malalamiko kwa wachezaji wa Peru. 

Zambarano aliokoa mpira wa juu kwa guu lake la kulia lakini mwisho wa siku mguu ule ukaishia kutua mgogoni mwa Aranguiz aliyedondoka huku akijishika mgongoni, mwamuzi hakuwa na kingine cha kufanya zaidi ya kutoa kadi nyekundu.

TIMU ZILIVYOKUWA 

Chile (4-3-1-2): Bravo 6.5, Isla 7, Medel 6, Rojas 5.5, Albornoz 5 (Mena 46, 7), Vidal 6.5, Diaz 6 (D Pizarro 46, 6), Aranguiz 5.5, Valdivia 7 (Gutierrez 86); E Vargas 8, Sanchez 6.5 

Peru (4-4-2): Gallese 6, Advincula 7, Zambrano 5, Ascues 6.5, Vargas 6.5, Carrillo 7 (C Pizarro 73, 6), Ballon 6.5, Lobaton 6 (Yotun 73, 6), Cueva 5 (Ramos 27, 6), Farfan 7, Guerrero 7.5

Peru wakasawazisha dakika ya 60 baada ya Gary Medel kujifunga katika juhudi zake za kuokoa.

Furaha ya Peru ikadumu kwa dakika nne tu kabla ya Eduardo Vargas mshambuliaji wa zamani wa QPR hajafunga tena katika dakika ya 64.  

Mshambuliaji wa Peru Paolo Guerrero alisema: "Sitaki tena kuzungumzia kuhusu waamuzi, siku zote wameonyesha wako upande wa wenyeji."

Peru sasa watacheza katika mechi ya kusaka mshindi wa tatu siku ya Ijumaa kati ya Argentina au Paraguay. 
Eduardo Vargas scored twice                  on Monday night to help Chile through to the Copa                  America final with victory over PeruEduardo Vargas amefunga  mara mbili dhidi ya Peru na kuisadia Chile kutinga fainali ya Copa America 
The former QPR loanee struck                  a superb winner into the top corner from well outside                  the box at the National Stadium
Eduardo Vargas akipiga shuti kufunga bao la pili kwenya Uwanja wa Taifa jijini Santiago
Kipa wa Peru  Pedro Gallese akiruka bila mafanikio huku mpira ukitinga wavuni
Carlos Zambrano caught Chile                  midfielder Charles Aranguiz on the back with his studs                  in the first half in SantiagoMguu wa Carlos Zambrano  ukienda mgongoni mwa Charles Aranguiz 
Hatimaye mguu unatua mgongoni 
The Peruvian defender was                  booked earlier on in the contest but was still shown a                  straight red card by referee Jose Argote
 Carlos Zambrano  anakula red card dakika ya 20
The Chile players celebrate                  at the end of the game - they will play either Colombia                  or Argentina in the Copa America final
Wachezaji wa  Chile wakishangilia baada ya mpira kumalizika
The Chile players gather                    in a huddle before the start of the game in front of                    their expectant home fans
Wachezaji wa  Chile wakiomba dua muda mfupi kabla mchezo hajaanza



Comments