Chelsea imeanzisha mazungumzo na Stoke City            juu kumpata kipa Asmir Begovic.
        Masaa machache baada ya safari ya Petr Cech            kwenda Arsenal kuthibitshwa, Chelsea imeanza kusaka mrithi            wake ambapo Jose Mourinho anamuona mlinda mlango huyo wa Bosnia kama mtu            sahihi.
        Daily Mail la Uingereza linafichua            kuwa Chelsea imepeleka ofa ya pauni milioni 6 kwaajili ya Asmir Begovic.
        Hata hivyo inaaminika Stoke itakataa ofa            huyo kutokana na ukweli kuwa inahitaji pauni milioni 10 ili            kumwachia kipa huyo.
        Mabingwa wa Premier                League  Chelsea wameanzisha maongezi na Stoke juu ya kipa                Asmir Begovic
        Jose Mourinho                anamchukulia Begovic kama mtu sahihi wa kuziba nafasi ya                 Cech aliyetimkia Arsenal
        
Comments
Post a Comment