CARLOS BACCA ATUA AC MILAN NA KUZIACHA KWENYE MATAA MANCHESTER UNITED NA LIVERPOOL



CARLOS BACCA ATUA AC MILAN NA KUZIACHA KWENYE MATAA MANCHESTER UNITED NA LIVERPOOL
Carlos                Bacca has agreed a deal with AC Milan, ending Liverpool's                pursuit in the Colombian striker


CARLOS BACCA amezipiga chini miamba ya Premier League - Liverpool na Manchester United na kuamua kujinga na AC Milan ya Italia.
Bacca amekubali dili hilo baada ya AC Milan kuweka mezani pauni milioni 21.5 ambazo zimetosha kufikia kipengele cha manunuzi kilichowekwa kwenye mkataba wake.
"Carlos amechagua kilicho bora kwa maisha yake, ana furaha kubwa"
Sergio Barila
Ripoti kutoka Italia zinasema Carlos amepewa ofa ya pauni milioni 1.8 kwa mwaka ambayo inaweza ikaongezeka hadi 2.5 kama atang'ara San Siro.
Nathibitisha kuwa Milan na mchezaji wamefikia makubaliano," Sergio Barila, mwakilishi wa Bacca aliliambia gazeti la Milan News la nchini Italia.
"Bacca amechagua kilicho bora kwa maisha yake, ana furaha kubwa. Itachukua muda gani dili kukamilika? hilo sasa waulizeni AC Milan," anaeleza Sergio Barila
Liverpool na Manchester United walikuwa wakimwania mshambuliaji huyo aliyeifungia Sevilla magoli 28 msimu uliopita.


Comments