Petr Cech amekamilisha              rasmi usajili wake Arsenal baada ya kufuzu vipimo vya afya              na akasema bado ana njaa ya mafanikio.
          Kipa huyo mwenye umri wa              miaka 33 anatua Arsenal kwa ada ya pauni milioni 10 baada ya              kuitumikia Chelsea kwa miaka 11. 
                                      "Petr Cech amethibitisha                    kuwa ni mmoja wa makipa bora duniani na atatuongezea                    nguvu kwenye kikosi chetu"
            Arsene Wenger
          Muda mfupi              baada ya kutambulishwa rasmi Arsenal, Cech akasema anafurahi              kujiunga na timu kubwa kama Arsenal na anashindwa kusubiri              siku ya kuanza maandalizi ya msimu mpya akiwa na timu yake              mpya.
          Cech alisema:              "Nina furaha sana kujiunga na Arsenal, wajibu wangu katika              soka ni ule ule, ari ile ile na njaa ile ile ya mafanikio              niliyokuwa nayo tangu nilipoanza maisha yangu ya soka.
          "Namshukuru sana              kocha Arsene Wenger kwa kuamini kuwa ninaweza kuwa kwenye              mipango yake, mara ya kwanza aliponiambia kuwa ananihitaji              nilifurahi na sikuwa na ubishi."
          Naye Arsene              Wenger alisema: "Katika misimu mingi,  Petr Cech              amethibitisha  kuwa ni mmoja wa makipa bora duniani na              atatuongezea nguvu kwenye kikosi chetu.
          "Petr Cech ni              mchezaji niliyemtamani kwa muda mrefu na nina furaha kuwa              amekubali kujiunga nasi."
                       
Comments
Post a Comment