Arsenal inaangalia uwezekano wa                kumtumia  mshambuliaji wake Alexis Sanchez              kumshawishi mchezaji mwenzake wa Chile Arturo Vidal kutua              Emirates.
          Washika bunduki wa London wanatajwa kuwa              wapo tayari kuweka mezani pauni milioni 21.3 kwa Juventus              ili kumpata Vidal.
          Kwa mujibu wa habari kutoka Hispania,              Sanchez amekuwa akifanya juhudi za kumvuta Vidal Arsenal              huku ikidawa Juventus wako tayari kumpiga bei kama pesa nene              itawekwa mezani.
          Kwasasa nyota hao wawili wako pamoja              wakiitumikia Chile kwenye michuano ya Copa America.
        Bosi wa Arsenal, Arsene                  Wenger  anaangalia namna ya kuboresha safu yake  ya                  kiungo na ulinzi ili kupigania vema mataji msimu ujao. 
          Vidal, 28 amekuwa na kiwango                  cha hali ya juu kwa muda mrefu tangu alipokuwa                  akiicheza Bayer Leverkusen ya              Ujerumani kabla hajahamia Juventus mwaka 2011. 
          
Comments
Post a Comment