ARSENAL YAMTIA MKONONI VIDAL KWA PAUNI MILIONI 21



ARSENAL YAMTIA MKONONI VIDAL KWA PAUNI MILIONI 21
Tetesi mpya za usajili ligi kuu ya England zinasema Arsena imefikia makubaliano ya kumsajili kiungo wa Chile na Juventus Arturo Vidal mwenye umri wa miaka 28.
Kwa mujibu wa gazeti la  La Stampa, la Chile, Vidal ameuzwa Arsenal kwa pauni milioni 21.
DONE DEAL? Vidal njiani kutua Arsenal 
Gazeti hilo limeeleza kuwa usajili wa kiungo huyo mwenye nguvu, bingwa wa kuharibu mipango ya timu pinzani na mmaliziaji mzuri anapokuwa jirani na goli la adui, atatangazwa rasmi muda mfupi baada ya michuano ya Copa America kumalizika wiki ijayo.
Juventus tayari wameshamsajili Sami Khedira kama mbadala wa Vidal na pia wahahitaji kuuza mchezaji kabla hawajasili chaguo lao lingine.
Mabingwa hao wa Italia wanataka kumsajili Mehdi Benatia kutoka Bayern Munich ili kuimarisha zaidi safu yao ya ulinzi.
Vidal ni kiungo anayesakwa zaidi na vilabu vingi barani Ulaya baada ya kuwa na misimu mitatu ya mafanikio Turin.
Msimu uliopita, Vidal alikuwa chaguo kuu la kocha wa Manchester United, Van Gaal lakini Juventus wakakataa kumuuza.



Comments