ARSENAL WATAJUTA KUMUUZA DAVID OSPINA …maajabu yake Copa America yaacha simulizi



ARSENAL WATAJUTA KUMUUZA DAVID OSPINA …maajabu yake Copa America yaacha simulizi
Colombia imetolewa na Argentina kwa njia ya 'matuta' kwenye robo fainali ya Copa America, lakini kama kuna mtu aliyelazimisha mechi hiyo iende hatau ya mikwaju ya penalti basi ni kipa wa Colombia David Ospina.
Ospina ambaye pia ni mlinda mlango wa Arsenal aliwanyima Argentina magoli mengi ya wazi kwa kupangua michomo mingi kwa namna ya ajabu.
Kipa huyo ambaye yuko njiani kuondoka Arsenal kufuatia ujio wa Petr Cech, aliokoa kwa mguu mkwaju wa Auguero ambao dhahiri ulikuwa unakwenda kutinga wavuni.
Ospina akawaduwaza watu pale alipopangua mpira wa kichwa wa Lionel Messi, kabla kumnyima goli Nicolas Otamendi.
Argentina walitawala mpira kwa muda wote wa mchezo lakini kipa David Ospina alikuwa kikwazo kwao.
Kwa muda wote wa michuano ya Copa America, Ospina amekuwa kwenye kiwango cha hali ya juu, hali inayotoa picha mbili – ya kwanza ni kwamba bei yake lazima ipande na ya pili Arsenal lazima watajuta kumuuza.
Ni wazi kuwa kipa huyu mwenye umri wa miaka 26 atakuwa mmoja wa makiba bora duniani.
David Ospina makes the                  second stop of an astonishing double save to palm away                  Lionel Messi's point-blank header
David Ospina akizuia mpira wa kichwa wa  Lionel Messi 
Aguero looks on in disbelief                  after watching Messi's instinctive header saved in                  acrobatic fashion by a flying Ospina
Aguero haamini kuwa mpira wa Messi umechezwa na Ospina
Messi and Aguero can't quite                  believe what they've seen as Ospina looks to the skies                  and Angel di Maria trudges off to take a corner
Messi na Aguero ni kama hawaani kinachotokea kwa Ospina huku Angel di Maria akienda kupiga mpira wa kona
Messi reacts with disbelief                  after Ospina saved his header with the goal gaping to                  keep the game scoreless
Messi akiduwaa kwa ubora wa Ospina 
Nicolas Otamendi rues his                  misfortune after Ospina saved his flicked effort from a                  corner and Cristian Zapata cleared off the lineNicolas Otamendi akilaani baada ya  Ospina kumnyima bao
Ospina was once again in the                  thick of things as he dives at the feet of Javier                  Pastore to thwart the tricky midfielderOspina anaruka mbizi kuzuia  Javier Pastore asilete madhara
The Arsenal keeper made up                  for a mistake in possession, reacting sharply to clear                  from the onrushing Aguero
Kipa wa  Arsenal alifanya kosa la kumiliki mpira lakini akawa mwepesi  kumzuia  Aguero asifunge





Comments