ALIYEMPIGA DOLE CAVANI AFUNGIWA ...SASA ATAKOSA MECHI ZOTE ZILIZOSALIA ZA COPA AMERICA


ALIYEMPIGA DOLE CAVANI AFUNGIWA ...SASA ATAKOSA MECHI ZOTE ZILIZOSALIA ZA COPA AMERICA
Beki wa Chile Gonzalo Jara amefungiwa baada ya kumtia dole mshambuliaji wa Uruguay Edinson Cavani kwenye mchezo wa robo fainali ya Copa America.

Jara alinusurika kupewa adhabu na mwamuzi wakati Cavani akilambwa kadi nyekundu baada ya kuhamaki na kumsukuma beki huyo. 

Ushahidi wa picha umemtia hatiani Jara na sasa atakosa michezo yote iliyosalia hata kama Chile itasonga mbele hadi fainali.

Jara alimlamba kofi la kishkaji Cavani kabla ya sekunde chache baadae hajamtia dole mshambuliaji huyo wa PSG.

Cavani  alihamaki, akamsukuma kidogo Jara ambaye alikuwa mwepesi kuzuga na akajitupa chini. Cavani  akapewa kadi ya pili ya njano na kutolewa nje.
Kutolewa kwa Cavani dakika ya 63 kuliiathiri Uruguay iliyojikuta inafungwa bao pekee dakika ya 81.

Hili ndio dole lililoleta balaa
Edinson Cavani (third left)                  makes his views very clear as he argues with Gonzalo                  Jara over the incidents
Edinson Cavani (watatu kushoto) akilalamika baada ya kuzinguliwa Gonzalo Jara 
Jara                    approached Cavani late in the game He                    appeared to stick his finger in the striker's bum
Jara anamsogelea Cavani na kumpiga dole
Jara then theatrically falls                  to the ground after a light flick in the face from the                  PSG striker
Jara anajiangusha na kumsababishia kadi nyekundu Cavani
Cavani was shown a red card                  for two yellows after abusing the referee's assistant                  and the flick at Jara
Cavani analambwa kadi nyekundu



Comments