MANCHESTER UNITED bado inapambana kwa            nguvu zote kuweza kukamilisha uhamisho wa mpachika mabao nyota            wa Lyon ya Ufaransa, Alexandre Lacazette.
        Mashetani hao wekundu wamevutiwa zaidi na            uwezo mkubwa wa kucheka na nyavu ulioonyeshwa na mshambuliaji            huyo msimu huu, ambapo alitikisa nyavu za adui mara 32.
        Straika huyo wa kimataifa wa Ufaransa            aliyeibuka kinara wa mabao katika Ligue 1, anafukuziwa na            klabu kadhaa barani Ulaya.
        Kwa mujibu wa mtandao wa FIchajes.net,            Lacazette atatangaza uamuzi juu ya mustakabali wake wiki ijayo            baada ya kumaliza mapumziko ya mwisho wa msimu.
        
Comments
Post a Comment