MABINGWA wa soka Tanzania            bara, Young Africans wametangaza kumaliza usajili wa wachezaji            wa ndani na sasa wanaangalia wa kimataifa.
        Katibu mkuu wa Yanga, Dr.            Jonas Tiboroa amesema wachezaji wa ndani waliowasajili mpaka            sasa wanatosha na wanachosubiri ni majibu kutoka TFF juu ya            mapendekezo waliyowasilisha wakiomba kuongeza idadi ya            wachezaji wa kigeni.
        Yanga wamependekeza            usajili wa wachezaji wa kigeni angalau ufikie idadi ya            wachezaji nane (8).
        "Wachezaji wa ndani            tuliosajili wanatosha, sasa hivi kinachotukwamisha kidogo ni            kauli kutoka kwa wenye mpira nchini TFF juu wachezaji wangapi            wa kigeni tunaruhusiwa kusajili". Amesema Dr. Tiboroa na            kuongeza: "
         "Malengo yetu mwaka huu            ni kuongeza uzoefu kidogo kwa maana ya kupata wachezaji wengi            wa nje na kutengengeza kikosi imara zaidi ya kile            kilichopita".
        Mpaka sasa Yanga            imesajili wachezaji watatu wa ndani ambao ni kiungo            mshambuliaji kutoka Mbeya City fc, Deus Kaseke, mlinda mlango            kutoka Kagera Sugar, Benedictor Tinocco na mlinzi wa kushoto            Mwinyi Hajji kutoka KMKM.
        
Comments
Post a Comment