TIMU ya Taifa ya Tanzania,            'Taifa Stars' imeanza vibaya michuano ya Cosafa baada ya            kukubali kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Swaziland katika mechi            ya michuano hiyo iliyomalizika usiku huu uwanja wa Royal            Bafokeng Sports Palace, Afrika kusini.
          Stars walifungwa goli hilo kutokana na makosa ya safu ya            ulinzi hususani upande wa kushoto alikocheza Oscar Joshua.
          Hata hivyo Stars walijitahidi kucheza vizuri na            kutengeneza nafasi nyingi ambazo washambuliaji wake John            Bocco, Mrisho Ngassa, Said Ndemla, Simon Msuva walishindwa            kuzitumia vizuri.
          Baada ya kichapo hicho, Stars wanarudi kujiwinda na            mchezo wa pili utakaopigwa mei 20 mwaka huu katika uwanja huo            huo dhidi ya Madagascar majira ya saa 11:00 jioni kwa saa za            Afrika kusini, sawa na saa 12:00 jioni kwa saa za Afrika            mashariki.
          Swaziland wao watachuana na Lesotho katika mechi ya pili            ya kundi B.
          Michuano ya Cosafa itaendelea kesho kwa mechi mbili,            Shelisheli watachuana na Zimbabwe majira ya saa 11:00 jioni            kwa saa za Afrika kusini sawa na saa 12:00 jioni kwa saa za            Tanzania, baadaye majira ya saa 1:30 usiku kwa saa za 'Sauzi'            sawa na saa 2:30 usiku kwa saa za Tanznaia, Namibia            watakabiliana na Mauritius.
Comments
Post a Comment