SUNDERLAND WAPAKI BUS NA KUITIBULIA ARSENAL ...VIJANA WA WENGER SASA MASHAKANI KUMALIZA NAFASI YA NNE ...pata picha kibao za mechi hiyo ya Ligi Kuu
Arsenal na Sunderland                    wametoshana nguvu katika mchezo wa Ligi Kuu                    uliomalizika kwa sare ya 0-0 kwenye dimba la Emirates Stadium.
              Sare hiyo imetosha kwa                    Sunderland ambayo sasa imejihakikishia kubaki Ligi                    Kuu, hatua iliyomfanya kocha Dick Advocaat atoe chozi la                    furaha.
              Kocha huyo wa Sunderland                    inabidi amshukuru kipa Costel Pantilimon ambaye aliokoa michomo                    mingi ya wazi huku Steven Fletcher akipoteza moja ya nafasi adimu                    kwa wageni baada ya kupaisha mpira akiwa katika eneo                    zuri la kufunga.
              Sunderland walipaki bus kwenye lango                  lao wakionekana wazi kutafuta sare.
              Kama Arsenal watapoteza mchezo wao wa                  mwisho na kisha Manchester United wakaifunga Hull City                  Jumapili, basi vijana wa Wenger wanaweza kujikuta                  wakimaliza katika nafasi ya nne.
               Olivier                    Giroud akichuana na John O'Shea
               Steven Fletcher wa              Sunderland akikosa boa la wazi 
        Kipa Ospina wa Arsenal              anapangua mpira ulipigwa na Fletcher 
         Santi Cazorla              akichuana na Connor Wickham 
         Jack Wilshere              akikabiliana na  Defoe 
         Fletcher jino kwa jino              na beki Laurent Koscielny 
        Aaron Ramsey akilambwa              kadi ya njano na refa Anthony Taylor katika kipindi cha              kwanza
         David Ospina              akiondosha hatari nyingine
        Theo Walcott apiga              shuti lakini kipa Pantilimon anaondoa
        Sunderland right back              Jones sticks a leg out to block Giroud's cross into the box              from the left
        Arsenal defender Per              Mertesacker and Sunderland striker Danny Graham chase down a              loose ball
        Winga wa Sunderland              Adam Johnson akikota mpira mbele ya Mesut Ozil wa Arsenal
        Nahodha wa Sunderland              O'Shea akimvuta jezi Giroud 
        Boss wa Arsenal, Arsene              Wenger akiwa hana la kufanya
        Kocha wa Sunderland              Dick Advocaat akitoa maelekezo
        
Comments
Post a Comment