SADIO MANE RAIA WA SENEGAL ANAYEWEKA HISTORIA MPYA PREMIER LEAGUE HUKU SOUTHMPTON IKIINYANYASA ASTON VILLA 6-0
Sadio Mane ameweka historia mpya            kwenye Premier League  baada ya kufunga mabao matatu            (hat-trick ) ya haraka zaidi kuliko wakati wowote ule katika            ligi hiyo.
        Hiyo ilikuwa ni katika mechi ya maangamizi            kwa Aston Villa iliyopokea kipigo cha 6-1 kutoka kwa            Southampton.
        Magoli matatu ndani ya dakika mbili na            sekunde 56 kutoka kwa winga huyo raia wa Senegal, lilikuwa ni            jambo la kuduwaza.
        Matokeo hayo yanaiweka Southampton kwenye            nafasi nzuri ya kucheza Europa League msimu ujao huku Aston            Villa ikisogea kwenye ukanda wa janga la kushuka daraja.
        Sadio Mane alifunga magoli hayo katika              dakika ya 13,              14 na 6 huku magoli mengine ya Southampton yakifungwa na Shane Long aliyefunga              mara mbili pamoja Graziano Pelle wakati              bao pekee la Aston Villa lilifungwa na Christian              Benteke.
        Sadio Mane akishangilia              rekodi mpya aliyoweka Premier League 
        Wachezaji wa              Southampton wakimpongeza Mane 
        Alan Hutton akishindwa              kumzuia Mane asifunge bao la kwanza
        Mane akitupia la pili
        Bao la tatu la Mane
        
Comments
Post a Comment