Mshambuliaji wa Liverpool Raheem Sterling ameingia kwenye hatua mpya ya sakata lake la kutimka Anfield baada ya kuelezwa kuwa nyota huyo yuko njiani kutafuta changamoto mpya.
Inadaiwa Sterling mwenye umri wa miaka 20 tayari ameweka sokoni nyumba yake iliyoko Merseyside, hali inayozidi kupalilia moto wa tetesi za kuondoka kwake.
Hatima ya Sterling Anfield imekuwa iking'ining'ia baada ya kukataa kusaini mkataba mpya hadi msimu umalizike kwanza.
Kukosa nafasi ya Liverpool kwenye Ligi ya Mabingwa msimu ujao, kunachukuliwa kama pigo lingine kwa kocha Brenden Rodgers katika harakati zake za kuhakikisha winga wake huyo anabakia katika kikosi chake.
Arsenal na Chelsea zinahusishwa kwa karibu sana na usajili wa Raheem Sterling.
Hatma ya Raheem Sterling ndani ya Liverpool iko mashakani
Raheem Sterling anahusishwa na Chelsea au Arsenal
Comments
Post a Comment