Mgomo wa La Liga wasitishwa



Mgomo wa La Liga wasitishwa

Barcelona's Messi is chased by Real Madrid's Ronaldo              during their Spanish first division "Clasico"              soccer match at Nou Camp stadium in Barcelona

Ligi kuu ya Hispania sasa itaweza kuendelea tena wikiendi hii baada ya kusitishwa kwa wiki nzima  na Shirikisho la Mpira wa Miguu  la Hispania (Spanish Football Federation – RFEF) na mgomo wa wachezaji kuisha.

Baada ya Mahakama Kuu ya Hispania kusema kuwa mgomo wa wachezaji  kuhusu haki za televisheni si  halali/si wa kisheria (unlawful),  Shirikisho nalo lilibadilisha kauli yake kwamba 'msimu umeisha'

Barcelona inaweza kushinda taji la  La Liga  Jumapili hii, kabla mechi ya mwisho haijachezwa, endapo itawafunga mabingwa, Atletico Madrid.

Mechi ya Kombe la Mfalme nayo itachezwa kama ilivyopangwa, tarehe 30 Mei. Barca – ambao pia wamefikia fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya, watakayovaana na kibibi kizee cha Turin, Juventus – watacheza na Athletic Club Bilbao kwenye Uwanja wa nyumbani, Camp Nou kwenye fainali hiyo ya Kombe la Mfalme.

 

Mwandishi habari za soka nchini Hispania, Andy West anaelezea mgogoro huu:

"Kimsingi, usitishwaji  wa ligi ulikuwa ni matokeo ya vita ya madaraka juu ya nani anaendesha mpira wa Hispania. Ni dhahiri kabisa, hiki ni kilele cha mgogoro wa muda mrefu juu ya mgawanyo wa mapato ya televisheni ambayo yamekuwa yakipimwa kwa kuwapendelea 'wakubwa wawili'  wa Barcelona na Real Madrid."

Shirikisho na umoja wa wachezaji (AFE) zimeridhika na sheria mpya inayojumuisha majadiliano ya bei juu ya haki za televisheni kwa mechi za ndani , inayoungwa mkono pia  na wasimamizi wa  Ligi ya Mpira wa Kulipwa nchini humo (National Professional Football League – LFP), inayoendesha ligi mbili kubwa za kulipwa nchini humo.

Wachezaji waliounga mkono mgomo wanaamini mgawanyo wa pesa  kwenye mkataba mpya uliopendekezwa na LFP na serikali ya Hispania hauwanufaishi wale wanaozichezea klabu za chini/ ndogo.

Ijumaa iliyopita, Raisi wa LFP, Javier Tebas alitangaza mipango ya kwenda mahakamani dhidi ya usitishwaji wa ligi, huku akionya italeta hasara ya mapato hadi  € 50 milioni (zaidi ya bilioni mia, shilingi za Tanzania) kwa mechi za mzunguko mmoja.

 

 

Hii  Ndio  Ratiba  ya  Mechi  Kali  Zilizobaki  Hispania.

 

Jumapili, 17 Mei: Atletico Madrid   v   Barcelona

                             Espanyol   v   Real Madrid

 

Jumamosi, 23 Mei: Barcelona   v   Deportivo

                                Real Madrid   v   Getafe

 

Jumamosi, 30 Mei: Fainali ya Kombe la Mfalme

                                Athletic Bilbao   v   Barcelona



Comments