MANCHESTER UNITED YATAKA PAUNI MILIONI 29 NA COENTRAO JUU ILI KUMUUZA DE GEA KWA REAL MADRID



MANCHESTER UNITED YATAKA PAUNI MILIONI 29 NA COENTRAO JUU ILI KUMUUZA DE GEA KWA REAL MADRID
Imedaiwa kuwa Manchester United wanataka walipwe na Real Madrid pauni milioni 29 ili kumwachia kipa David de Gea.
Imeripotiwa kuwa De Gea amekubaliana na Real Madrid juu ya maslahi yake binafsi katika dili linalotajwa kufikia zaidi ya pauni milioni 3.6 kwa mwaka, lakini miamba hiyo ya Hispania bado haijakubaliana na Manchester United juu ya usajili wa kipa huyo mwenye umri wa miaka 24 ambaye amebakiza miezi 14 ya mkataba wake Old Trafford.
Gazeti la Marca la Hispania limedai United inataka pauni milioni 28.6 kwa kipa huyo kwa kimataifa wa Hispania lakini pia kukiwa na sharti la kupewa beki wa kushoto Fabio Coentrao.
David de Gea applauds the                    Manchester United fans during the 1-1 draw with                    Arsenal on Sunday   The Spaniard has been                      linked with a move to Real Madrid
David de Gea akiaminika kuwa alikuwa anawaaga mashabiki wa  Manchester United katika mchezo dhidi ya Arsenal Jumapili iliyopita
De Gea was taken off injured                  during the game at Old Trafford as United fans urged him                  to stay at the club
De Gea akiwapungia mashabiki wakati akienda benchi baada ya kuumia
Portuguese defender Fabio                  Coentrao (centre) has reportedly been offered to United                  as part of a swap deal
Beki wa Kireno Fabio Coentrao (katikati) anahusishwa katika dili la De Gea.







Comments