Imedaiwa kuwa Manchester United wanataka            walipwe na Real Madrid pauni milioni 29 ili kumwachia kipa            David de Gea.
        Imeripotiwa kuwa De Gea amekubaliana na            Real Madrid juu ya maslahi yake binafsi katika dili            linalotajwa kufikia zaidi ya pauni milioni 3.6 kwa mwaka,            lakini miamba hiyo ya Hispania bado haijakubaliana na            Manchester United juu ya usajili wa kipa huyo mwenye umri wa            miaka 24 ambaye amebakiza miezi 14 ya mkataba wake Old            Trafford.
        Gazeti la Marca            la Hispania limedai United            inataka pauni milioni 28.6 kwa kipa huyo kwa kimataifa wa            Hispania lakini pia kukiwa na sharti la kupewa beki wa            kushoto Fabio Coentrao.
        David de Gea akiaminika              kuwa alikuwa anawaaga mashabiki wa  Manchester United katika              mchezo dhidi ya Arsenal Jumapili iliyopita
        De Gea akiwapungia              mashabiki wakati akienda benchi baada ya kuumia
        Beki wa Kireno Fabio              Coentrao (katikati) anahusishwa katika dili la De Gea.
        
Comments
Post a Comment