Kwa mashabiki wa Manchester United            waliokuwa wakifuatilia mechi ya nusu fainali ya Ligi ya            Mabingwa kati ya Real Madirid na Juventus kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu Jumatano usiku, watakuwa            wamefahamu ni kitu gani wanakikosa kwa kiungo Paul Pogba.
        United walimuona kiungo huyo bado hana            nafasi katika kikosi cha kwanza na matokeo yake akaondoka bure            mwaka 2012 na sasa anatinga fainali ya Ligi ya Mabingwa akiwa            na Juventus.
        Pobga aliambiwa awe mpole Old Trafford:            "Muda wako utawadia" hiyo ilikuwa ni meseji kutoka kwa kwa            makocha wa United wakimtaka asiondoke lakini haikusaidia.
        Juventus hawakuwa kwenye kiwango chao bora            katika mchezo huu ulioisha kwa sare ya 1-1, lakini Pobga            aliyekuwa anarejea kutoka kwenye maumivu yaliyomweka nje kwa            miezi miwili, aling'ara vilivyo.
        Paul Pogba (kulia)              akishangila na Claudio Marchisio 
        Pogba akidhibitiwa na              Daniel Carvajal 
        Pogba akimjaribu kipa              wa Real Madrid Iker Casillas
        
Comments
Post a Comment