Luis Figo alia na FIFA




Luis Figo alia na FIFA
fifaaa
Luis Figo amesema "soka limepotea" baada ya Sepp Blatter kuchaguliwa tena kuwa rais wa Fifa jana na kumtaka kwa mara nyingine tena kuondoka katika nafasi hiyo.
Blatter (79) alimshinda mpinzani wake Prince Ali kutoka nchini Jordan, ambapo sasa atakaa tena madrakani kwa miaka minne mingine huku akiwa amekaa madarakani kwa takribani vipindi 5.
Blatter alipata kura 133 dhidi ya 73 za Prince Ali kabla ya mpinzani wake huyo kuamua kujitoa katika raundi ya pili.
Ushindi wake umekuja huku viongozi 14 wa shirikisho hilo wakiwa wamekamatwa kwa tuhumu za rushwa siku chache tu kabla ya uchaguzi.
Figo – ambaye hapo awali alipanga kuwania nafasi hiyo kabla ya kujitoa kwa madai ya kutozigawa kura ili kurahisisha kumng'oa Blatter, amesema kuwa amehuzunishwa sana na matokeo ya uchaguzi huo.
"Leo ilikuwa ni siku nyngine ya giza hapa Zurich," alisema nguli huyo wa Ureno. "Fifa imepotea, lakini juu ya yote hayo, soka limepotea na kila mpenda soka amepotea pia.
"Blatter alitoa sababu za kijinga sana pale aliposema hawezi kudhibiti kila mtu ndani ya shirikisho. Hilo ni kama tusi kwa wapenda soka. Hawa watu, ambao Blatter amekuwa akiwatunuku vyeo kwa miaka kadhaa, leo anawageuka, Fifa sio shirikisho lenye maadili tena.
"Kama Blatter alihusika kwa udogo katika soka, basi sidhani kama angechaguliwa. Kama ana upungufu wa maadili, basi ndani ya miaka michache ijayo atajiuzulu."


Comments