KOCHA mkuu wa Taifa            Stars, Mart Nooij baada ya jana kuchapwa goli 1-0 na Swaziland            katika mechi ya ufunguzi ya mechi ya Cosafa ameamua kutoa            shukurani kwa kualikwa.
        Nooij amesema anashukuru            kwa kupata mwaliko huu, kwani kwake anatumia michuano hii kama            sehemu ya maandalizi ya kuwania kufuzu kwa fainali za mataifa            Afrika (AFCON, CHAN) mwezi juni.
        Kocha huyo  anaamini            wachezaji aliowaacha majeruhi nyumbani pamoja na wachezaji wa            kimataifa wanaochezea klabu ya TP Mazembe, wataongeza nguvu            katika kikosi chake watakaporejea Tanzania.
                Baadhi ya watanzania            waishio nchini Afrika Kusini walijitokeza uwanja wa Royal            Bafokeng kuishangilia timu ya Taifa ya tanznaia Taifa Stars            wakiwa sambamba na maofisa wa ubalozi wa Tanzania nchini            Afrika Kusini.
        Taifa Stars itacheza            mchezo wake wa pili siku ya jumatano saa 11 za jioni kwa saa            za Afrika kusini, sawa na saa 12 jioni kwa saa za Afrika            Mashariki dhidi ya Madagascar katika uwanja wa Royal            Bafokeng., ambao katika mchezo wa awali wamibuka na ushindi wa            mabao 2-1 dhidi ya Lesotho.
                Wakati huo huo kiungo wa            Taifa Sars Said Juma "Makapu" ambaye anasumbuliwa na majeruhi,            anatarajiwa kurejea nyumbani Tanzania leo kwa ajili ya kupata            vipimo zaidi na matibabu.
        

Comments
Post a Comment