UKURASA rasmi wa                facebook wa  Juventus amejibu mapigo kwa wale wote                waliokuwa wanawabeza baada ya kufika nusu fainali.
            Baada ya droo ya                mechi za nusu fainali za Uefa Champions League kutoka,                wengi waliwadharau Juventus na kuwaona wanyonge katika                timu nne zilizosalia.
            Wakicheza nusu                fainali kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2003, Juventus                wamewashangaza wengi baada ya kuwachapa mabingwa watetezi,                Real Madrid kwa ushindi wa jumla wa magoli 3-2.
            Miamba hiyo ya Italia                itakabiliana na Barcelona katika mechi ya fainali juni 6                mwaka huu mjini Berlin na wanatarajia kutwaa ubingwa wa                kwanza wa Uefa tangu walipofanya hivyo mwaka 1996.
            Ukurasa wa facebook                wa Juventus ume-post picha chache leo kuwajibu                waliowadharau kabla ya mechi za nusu fainali.
            Katika picha hizo                waliandika maneno yaliyosomeka ""Remember these?" yaani                Unakumbua haya?
            


14May2015
Comments
Post a Comment