JUVENTUS ‘YAINYIMA’ DUNIA FAINALI YA KIHISTORIA …Real Madrid yaishia nusu fainali



JUVENTUS 'YAINYIMA' DUNIA FAINALI YA KIHISTORIA …Real Madrid yaishia nusu fainali
Juventus defenders            Leonardo Bonucci and Giorgio Chiellini jump on Morata as Real            Madrid's players react to the goal in the background
Juventus imeinyima dunia kile kilichotarajiwa kuwa fainali kubwa kuliko zote za Ligi ya Mabingwa baada ya kulazimisha sare ya 1-1 kwa Real Madrid.
Hiyo inamaanisha kuwa ndoto ya Real Madrid kukutana na Barcelona kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya imeyeyuka na sasa ni Juventus wanaopenya kwenda Berlin. Hukuna tena fainali ya Barcelona na Real Madrid wala fainali ya Messi na Ronaldo.
Barcelona ilitangulia fainali baada ya kuitoa Bayern Munich kwa jumla ya bao 5-3.
Ronaldo aliipatia Real Madrid bao la kuongoza dakika ya 23 kwa njia ya penalti na kudumu hadi mapumziko.
Buffon watches on            helplessly after diving to his right as Ronaldo puts his            spot-kick straight down the middle
Mchezaji wa zamani wa Real Madrid Alvaro Morata alikuwa mwiba kwa mara ya pili kwa wenyeji baada ya kuisawazishia Juventus dakika ya 57.

Alvaro Morata  alifunga pia katika mchezo wa kwanza uliochezwa wiki iliyopita ambapo Juventus ilishinda 2-1.
Arturo Vidal (top) and            his Juventus team-mates mob Morata after his crucial strike in            the Champions League semi-final second leg
Real Madrid: Casillas, Carvajal, Sergio Ramos, Varane, Marcelo, Rodriguez, Kroos, Isco, Bale, Benzema, Ronaldo
Illarramendi
Juventus: Buffon, Lichtsteiner, Bonucci, Chiellini, Evra, Pogba, Pirlo (Barzagli 79), Marchisio, Vidal, Tevez, Morata (Llorente 84)


Comments