Juventus imeinyima dunia kile kilichotarajiwa kuwa            fainali kubwa kuliko zote za Ligi ya Mabingwa baada ya            kulazimisha sare ya 1-1 kwa Real Madrid.
        Hiyo inamaanisha kuwa ndoto ya Real Madrid kukutana na            Barcelona kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya            imeyeyuka na sasa ni Juventus wanaopenya kwenda Berlin. Hukuna            tena fainali ya Barcelona na Real Madrid wala fainali ya Messi            na Ronaldo.
        Barcelona ilitangulia fainali baada ya kuitoa Bayern            Munich kwa jumla ya bao 5-3.
        Ronaldo aliipatia Real Madrid bao la kuongoza dakika ya            23 kwa njia ya penalti na kudumu hadi mapumziko.
        Mchezaji wa zamani wa Real Madrid Alvaro            Morata alikuwa mwiba kwa mara ya pili kwa            wenyeji baada ya kuisawazishia Juventus dakika ya 57.
                                        Alvaro Morata  alifunga pia katika mchezo wa kwanza uliochezwa wiki            iliyopita ambapo Juventus ilishinda 2-1.
        Real Madrid: Casillas,            Carvajal, Sergio Ramos, Varane, Marcelo, Rodriguez, Kroos,            Isco, Bale, Benzema, Ronaldo
        Illarramendi
        Juventus: Buffon,            Lichtsteiner, Bonucci, Chiellini, Evra, Pogba, Pirlo (Barzagli            79), Marchisio, Vidal, Tevez, Morata (Llorente 84)
        
Comments
Post a Comment