FUJO ZA VAN GAAL ZAANZA, MAN UNITED YATUMA MAOMBI KUMSAJILI RAHEEM STERLING ...mwiko wa miaka 51 hatarini kuvunjwa
 
      Manchester United imepeleka maombi ya            kutaka kumsajili winga wa Liverpool Raheem Sterling.
        Hakuna mchezaji aliyewahi kukatiza moja kwa            moja baina ya timu hizo mbili zenye upinzani wa hali ya juu            tangu mwaka 1964 wakati Phil            Chisnall alipotoka United na kujiunga na Liverpool.
        Hata hivyo Liverpool wameiambia Manchester            United kuwa hawana mpango wa kumuuza nyota huyo wa kimataifa            wa England.
        Raheem amekataa kusaini mkataba mpya na            amemwambia wazi kocha wake Brendan            Rodgers kuwa anataka kuondoka Liverpool kiangazi hiki.
        Manchester United              imetupa ndoano kwa Raheem Sterling
        Sterling akiwasili              mazoezini Liverpool Jumatano jioni
        Sterling atakuwa              mchezaji wa kwanza kutoka Anfield kwenda United na kuvunja              mwiko wa miaka 51 wakati  Phil Chisnall alipojiunga na              Liverpool  1964 akitokea Old Trafford.
        
Comments
Post a Comment