CHELSEA SASA YAMTAKA FALCAO ...wakala wake ndiye wakala wa Jose Mourinho



CHELSEA SASA YAMTAKA FALCAO ...wakala wake ndiye wakala wa Jose Mourinho
Chelsea imeanzisha maongezi na Radamel Falcao pamoja na wawakilishi wake ili kuangalia uwezekano wa mshambuliaji huyo wa Colombia kutua Stamford Bridge.
Falcao alichemsha katika msimu mzima alioitumikia Manchester United kwa mkopo akitokea Monaco ambapo alifunga magoli manne tu katika mechi 29 alizocheza.
Kocha wa United Louis van Gaal  alithibitisha wiki iliyopita kuwa hawana mpango wa kumpa mkataba wa kudumu Faclao ambao ungeigharimu klabu hiyo ya Old Trafford pauni milioni 44.
Hata hivyo uwepo wa Falcao hapo United umeigharimu timu hiyo kiasi cha pauni milioni 40 kuanzia mshahara wake wa pauni 285,000 kwa wiki na ada ya pauni mil 6 ya kumchukua kwa mkopo.
Inaaminika Falcao yupo tayari kupunguza mshahara wake na tayari alishawaamuru wawakilishi wake wamtafutie timu nyingine ya Premier League.
Wakala wake Jorge Mendes amesema zipo dalili ya mteja wake kutua Stamford Bridge. Jorge Mendes  pia ndiye wakala wa kocha wa Chelsea wa Chelsea Jose Mourinho.  
Colombia captain Radamel                  Falcao is handed the national flag by President Juan                  Manuel Santos on Friday
Nahodha wa Colombia Radamel Falcao akikabidhiwa bendera na Rais wa nchi hiyo Juan Manuel Santos  siku ya Ijumaa 
Falcao's brief spell at Old                  Trafford is still believed to have cost Manchester                  United £40million
Falcao huenda akatua Chelsea 





Comments