Carlos Tevez anasemekana kuwa mbioni            kurudi katika Premier League huku akiripotiwa kuichagua            Liverpool kuwa kituo chake kipya.
        Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester            City, Manchester United na West Ham anaaminika kujiandaa            kufunga virago kuondoka Juventus kiangazi hiki.
        Ingawa hivi karibuni alitupilia mbali            taarifa kuwa anataka kuondoka Turin, gazeti la Telegraph            limeripoti kuwa staa huyo anazingatia ofa ya kujiunga na            Liverpool.
        Hata hivyo wataalam wa mambo wanaona suala            la Liverpool kukosa nafasi ya kucheza Champions League msimu            ujao linaweza kuwa kikwazo kwa Tevez.
        Kuondoka katika timu iliyoingia fainali ya            Ligi ya Mabingwa na kwenda kujiunga na timu iliyokosa nafasi            ya Champions League ni tatizo.
        
Comments
Post a Comment