MSHAMBULIAJI Jeryson            Tegete na kiungo Nizar Khalfan wamesajiliwa na timu mpya            iliyopanda ligi kuu soka Tanzania bara  msimu ujao, Mwadui fc.
        Kocha mkuu wa Mwadui,            Jamhuri Musa Kihwelo 'Julio' amethibitisha kuwasajili            wachezaji hao waliotemwa na Yanga na kila mmoja amesaini            mkataba wa mwaka mmoja.
        Julio amesema bado            anaendelea kufanya mazungumzo na wachezaji wengi wenye uzoefu            ili ligi ikianza kikosi chake kiwe na makali ya kutisha.
        
Comments
Post a Comment