ARSENAL YALA KIPORO KILICHOOZA, YAPIGWA 1-0 NA SWANSEA ...nafasi ya pili sasa hatarini, ya tatu nayo mashakani




ARSENAL YALA KIPORO KILICHOOZA, YAPIGWA 1-0 NA SWANSEA ...nafasi ya pili sasa hatarini, ya tatu nayo mashakani
Gomis rises to beat Arsenal left back Nacho Monreal and              Laurent Koscielny to head home the winning goal late on in              the match
Arsenal imeshindwa kutumia vizuri mchezo wake wa kiporo cha Premier League baada ya kulambwa na Swansea 1-0.
Bafetimbi Gomis aliifungia Swansea bao pekee zikiwa zimebakia dakika tano mpira kumalizika, akimalizia kwa kichwa krosi ya Jefferson Montero.
Bao hilo lilisaidiwa na teknolojia mpya ya goli baada kipa David Ospina kufanikiwa kuokoa mpira lakini ikabainika kuwa tayari ulishavuka mstari wa goli.
Arsenal sasa watakwenda Old Trafford Jumapili wakiwa na tahadhari kuwa kupoteza mchezo huo kunaweza kuwafanya wawe nyuma ya vijana wa Louis van Gaal.
Ingawa bado watakuwa na mchezo mmoja mkononi, lakini Arsenal watakuwa kwenye presha kubwa na iwapo watateleza basi nafasi ya tatu itakuwa mashakani, achilia mbali nafasi ya pili.
Kikwazo kikubwa kwa Arsenal kilikuwa ni kipa wao wa zamani Lukasz Fabianski ambaye aliondoa michomo mingi ya wazi ikiwemo ya Alexis Sanchez na Theo Walcott.
Siku zote Arsene Wenger alikuwa akiamini kuwa Lukasz Fabianski ni kipa bab kubwa na usiku huo wa Jumatatu mlinda mlango huyo akadhirisha hivyo.
Fabianski  aliondoka Arsenal kiangazi kilichopita licha ya Wenger kujitahidi kadri awezavyo kumshawishi abakie Emirates.
ARSENAL (4-2-3-1): Ospina 6; Bellerin 6, Mertesacker 6, Koscielny 6, Monreal 6; Coquelin 6 (Wilshere 60, 6), Cazorla 6.5; Ramsey 6.5, Ozil 6, Sanchez 6; Giroud 5 (Walcott, 6).
Manager: Arsene Wenger 6.
SWANSEA (4-1-4-1): Fabianski 8; Rangel 6 (Richards 60, 5), Fernandez 6.5, Williams 6.5, Taylor 6; Cork 6.5; Dyer 6 (Barrow), Shelvey 6, Ki 6 (Gomis), Montero 6; Sigurdsson 5.
Arsenal goalkeeper David                  Ospina tries in vain to stop Bafetimbi Gomis' effort                  crossing the line in the 86th minute
Kipa wa Arsenal  David Ospina akijaribu kuokoa mpira Bafetimbi Gomis ulizaa goli dakika ya 86
Referee Kevin Friend signals                  for a goal and points to his wrist device that informs                  him when the ball has crossed the line
Referee Kevin akionyesha kuwa hilo ni goli baada ya kubainika kuwa mpira ulivuka mstari
Mshambuliaji wa Kifarasan Bafetimbi Gomis akishangilia bao baada refa Kevin Friend kuthibitisha kuwa ni goli
Television replays on Sky Sports Monday Night Football              confirmed that the decision to award the goal was correct
Ni goli, hakuna ubishi
Fabianski saves from Giroud as Arsenal squander another              chance to take a first-half lead on a frustrating night in              north London
Lukasz Fabianski akiondoa moja ya hatari
Fabianski shakes hands with fellow Pole and Arsenal              substitute goalkeeper Wojciech Szczesny after the match 
Lukasz Fabianski  akisalimiana na kipa wa akiba wa Arsenal Wojciech Szczesny baada ya mchezo






Comments