ARSENAL YAANZA MDOGO MDGO KWENYE USAJILI, YANASA WAWILI KUTOKA UFARANSA ...ni eff Reine-Adelaide na Yassin Fortune wa Lens


ARSENAL YAANZA MDOGO MDGO KWENYE USAJILI, YANASA WAWILI KUTOKA UFARANSA ...ni eff Reine-Adelaide na Yassin Fortune wa Lens
Arsenal imefikia makubaliano na klabu ya Lens ya Ufaransa kwaajili ya kuwasajili machipukizi wake wawili Jeff Reine-Adelaide na Yassin Fortune.
Wachezaji wote wawili ni washambuliaji ambao pia wana uwezo wa kucheza kama viungo na wote waliiwakilisha Ufaransa kwenye michuano ya kimataifa ya U 17.
Daily Mail linaandika kuwa Fortune alikuwa anatakiwa na United lakini timu hiyo ya Old Trafford ikabwaga manyanga baada ya kutajiwa bei.
Lens imewauza wachezaji wote wawili kwa pauni milioni 3 pamoja na marupurupu kutokana na namna watakavyokuwa wakicheza kwenye kikosi cha kwanza.
Reine-Adelaide na Yassin Fortune wataungana na  Yaya Sanogo ambaye alihamia Emirates Stadium baada ya kung'ara Ufaransa.
Hata hivyo Sanogo ameshindwa kufurukuta England, Arsenal ikamtoa kwa mkopo kwenda Crystal Palace ambako nako ameshindwa kung'aa.
Arsenal manager Arsene Wenger is set to add Jeff                Reine-Adelaide and Yassin Fortune to his squad 
Arsene Wenger anawaongeza Jeff Reine-Adelaide na Yassin Fortune kwenye kikosi chake 
Fortune was linked with a move to Manchester                  United      Reine-Adelaide (left) will                  arrive with Fortune at Arsenal in a deal worth around                  £3million plus bonuses
Fortune (kushoto) na Reine-Adelaide (kulia) wanatua Arsenal kwa pauni milioni 3
The                duo join Yaya Sanogo in making the move to the Emirates                Stadium after impressing in France 
Reine-Adelaide na Yassin Fortune wataungana na  Yaya Sanogo ambaye alihamia Emirates Stadium baada ya kung'ara Ufaransa.



Comments