Mastaa wa Manchester            United wanahofia kwamba kipa wao namba moja, David De Gea            ataondoka Old Trafford na kujiunga na Real Madrid.
        Kipa huyo raia wa            Hispania amebakisha mwaka mmoja katika mkataba wake nab ado            hajasaini dili jipya Old Trafford licha ya juhudi za bodi ya            United na kocha Louis Van Gaal.
        Madrid inamtaka kipa            huyo mwenye umri wa miaka 24 kwenda kuchukua nafasi ya Iker            Casillas.
        Gazeti la Daily Mirror            limedai kuwa wachezaji wa United wamemshawishi kipa huyo            anayetaka kuondoka baada ya miaka minne. 
        Kama De Gea atatangaza            nia ya kuondoka, United inaelezwa kuwa itaikamua Madrid pauni            milioni 50.
        
Comments
Post a Comment